Psalms 105:1-6

Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli

(1 Nyakati 16:8-22)


1 aMshukuruni Bwana, liitieni jina lake,
wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

2 bMwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,
waambieni matendo yake yote ya ajabu.

3 cLishangilieni jina lake takatifu,
mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

4 dMtafuteni Bwana na nguvu zake,
utafuteni uso wake siku zote.


5 eKumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,
miujiza yake na hukumu alizozitamka,

6 fenyi wazao wa Ibrahimu mtumishi wake,
enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Copyright information for SwhKC