Psalms 105:1-6
Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli
(1 Nyakati 16:8-22)
1 aMshukuruni Bwana, liitieni jina lake,
wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
2 bMwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,
waambieni matendo yake yote ya ajabu.
3 cLishangilieni jina lake takatifu,
mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
4 dMtafuteni Bwana na nguvu zake,
utafuteni uso wake siku zote.
5 eKumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,
miujiza yake na hukumu alizozitamka,
6 fenyi wazao wa Ibrahimu mtumishi wake,
enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Copyright information for
SwhKC